<$BlogMetaData$>

 

HOME | PROFILE | GUEST BOOK | CONTACTS | MAKE IT YOUR HOME PAGE | MY FACE BOOK PAGE | MY JAMII FORUM PAGE | VIST MY PAGE @ TWITER
karibu katika JUKWAA HURU LA UCHAMBUZI, maskani ya uchambuzi na wachambuzi makini. Jisikie huru kuchangia mjadala wowote ulioko humu ndani pamoja na kutuma maoni, mawazo, au chochote unachodhani kuwa kinahitajika kujadiliwa na jamii kwa ujumla. Kutuma makala au habari au kuwasiliana nami, niandikie kupitia: msangirs@yahoo.co.uk
KARIBU SANA JUKWAAHURU.COM
Mwandishi: Ramadhani Msangi Tarehe: 12/02/2009 12:49:00 AM | kiungo mahususi

NI KWA MTAZAMO ULE ULE, MWELEKEO ULE ULE, KASI ILE ILE.... TOFAUTI NI MASKANI TU BASI.

WAPENDWA WADAU WA BLOGI HII, NAPENDA KUWATAARIFU RASMI KUWA, INAHAMIA KATIKA ANWANI MPYA YA http://www.jukwaahuru.com/.

ENDELEA KUNIFUATILIA MIMI NA WADAU WENGINE MBALIMBALI KATIKA MASKANI YANGU MPYA YA UCHAMBUZI YAKINIFU KWA KUBONYEZA HAPA
 
KWA CCM HII HII YA KUNG'ATA NA KUPULIZA!!
Mwandishi: Ramadhani Msangi Tarehe: 9/28/2009 02:02:00 PM | kiungo mahususi
Katibu mkuu wa CCM, Yusuph Makamba, ameunganga na mwenyekiti wa chama chake kitaifa, aliye pia rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Jakaya Kikwete, katika kututengenezea mwisho wa filamu ya kuchekesha yenye kuelezea matatizo ndani ya chama chao.

Wakati ambapo mheshimiwa JK, yeye alihitimisha kipande chake katika filamu hiyo akiwa jijini Dar es salaam, kwa staili ya kujibu maswali ya wananchi kupitia luningani, Makamba, yeye aliamua kumalizia kipande chake kule jimboni Urambo kwa staili ya kuhutubia wananchi kupitia mkutano wa hadhara.

Na kwakuwa kama zilivyo filamu zingine, hii nayo ilikuwa na script yake, bila shaka ndio maana haikuwa taabu kwa vigogo hawa kuwa na majibu ambayo yalishabihiana kwa karibu.Majibu ya kisanii.

Kwa Makamba ninayemjua, ambaye nimekuwa nikiamini kuwa anapoteza muda katika siasa ilhali tasnia ya sanaa ikiwa inamhitaji sana, hili lilikuwa jambo nililolitarajia. Ilikuwa suala la muda tu, ambao hatimaye aliupata na kuutumia vyema kama ilivyo ada kwake.

'Filamu' yenyewe ambayo sehemu kubwa ilichezwa mjini Dodoma, ilihusisha tukio linalomhusisha mtu mmoja ambaye kutokana na mapenzi yake kwa Watanzania wenzake, aliamua kusimama kidete katika upande wa kuwatetea.

Mhusika wa nafasi hii, Samwel 'a.k.a Standard and Speed' Sita, Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ambaye ni wazi kuwa amedhihirisha kasi na kiwango chake katika kulipa Bunge letu meno, alijikuta katika wakati mgumu kutokana na utendaji wake ambao kimsingi umekuwa ukizingatia ilani ya chama chake na kilicho pia chama tawala CCM.

Kuwaletea Watanzania maisha bora, kuimarisha mijadala yenye maslahi ya kitaifa ndani ya Bunge, kwa lengo la kuimarisha demokrasia, ni baadhi tu ya mambo yenye kuzungumzwa katika kila muongozo wa CCM, na ambayo Sitta, amekuwa akiyafanya.

Hata hivyo, ni mambo kama haya haya ambayo kada huyu mkongwe wa CCM, amekuwa akiyatekeleza kwa matendo, ambayo yalielekea kumponza.

Katika kile kilichoonekana kama kiashiria cha kiwango cha unafiki ulivyowajaa baadhi ya wana-CCM, na hususan watendaji wa ngazi za juu wa chama hicho, ilibakia almanusura Sitta, sio tu kuondolewa katika nafasi yake ya uspika bali pia kupokwa ubunge na uanachama wake katika CCM.

Taarifa za matukio haya yote zilikuwa wazi, ziliripotiwa na kusambaa kila kona ya nchi. Halikuwa kificho, lilikuwa jambo la wazi.

Kwamba baada ya vikao vile vya wakubwa kwisha hakukutolewa tamko lolote la kukanusha taarifa za kilichokuwa kimedhamiriwa kumkumba Sitta, ni ishara ya kuwa kweli kulikuwa na dhamira hiyo.

Tulimsikia Makamba, akiongea na vyombo vya habari, tena kwa lugha ya ukali, kuwa vikao hivyo vilikuwa na haki ya kufanya waliyoyafanya kwakuwa CCM ni zaidi ya kila mtu/kitu.

Kwamba CCM ni zaidi ya sheria za nchi, kwamba CCM ina haki ya kuvunja katiba ya nchi kwa kumhoji, kumdhalilisha na kutaka kumuwajibisha kiongozi mkuu wa mhimili wa nchi, kwa kutimiza wajibu wake ambao katiba ya nchi inamtaka kuutimiza.

Lakini katikati ya kiza kilichowashukia Watanzania juu ya uadilifu, uelewa, busara na utimilifu wa utendaji kazi walio nao viongozi na baadhi ya wana-CCM, wale waliostahili kuhakikisha unyoofu wa mambo, wakatujia na masimulizi ya kuvunja mbavu kwa vilio vya masikitiko.

Tukamsikia mwenyekiti wa CCM, mhe. Jakaya Kikwete, akituambia kuwa kilichojiri Dodoma, yalikuwa ni malumbano makali sana. Tukamsikia Makamba, akijinasibu kwa mama mzazi wa Spika wetu, kuwa hakuwa na matatizo na mh. Sitta.

Hakuna hata mmoja wao aliyetamka kuwa, taarifa za mzee wa viwango na kasi, alikuwa akizushiwa tu kuwa anataka kufukuzwa. Na hili linamaanisha kuwa ni kweli wana-CCM kupitia vikao vyao, walidhamiria kumtendea unyama huo.

Kwa Sitta, ambaye uadilifu wake kwa CCM, haujawahi kuwa jambo la kuhoji, kwa Sitta, ambaye mapenzi yake kwa CCM, yamemfanya aone kuwa chama kinaenda kubaya na kinahitaji kurejesha imani yake kwa wananchi na akaonyesha njia katika kurejesha imani hiyo, ni wazi kuwa yaliyotokea kule Dodoma, ulikuwa udhalilishaji mkubwa sana kwake.

Kwa mh. JK, kukaa kimya akaiachia hali ile akiwa ni mwenyekiti wa chama na akamnyamazia hata Makamba, aliyetoa kauli za kuhalalisha udhalilishaji ule, ni wazi kuwa, hata yeye alikuwa anayafurahia na kuyakubal.

Na kama mhe. JK, ameshindwa kuwakemea watu aina ya Makamba, ambao wanavunja katiba ya nchi kwa kuhoji utendaji wa Spika tenda ulio ndani ya muongozo sahihi kikatiba na kiilani ya CCM, ana sababu ipi ya kutufanya tuendelee kumuamini?

Hivi ikitokea Bunge nalo likaamua kumjadili raisi, kiasi cha kufikia kufikiri, angalau kufikiri tu, kuwa anatakiwa aondoke madarakani, atakaa kimya na kuyachekelea hayo?

Hapa ndipo ninapokumbuka alichowahi kuandika Ansbert Ngurumo, kuwa mh JK, ni kama mtu ambaye hawezi hata kuchinja kuku wake, kwakuwa anaogopa kurukiwa na damu, kwahiyo atatafuta mtu amsukumie mzigo huo.

Na hili ndilo alilolitenda kwa kuunda tume ya kuchunguza kiini cha malumbano baina ya wabunge wa CCM. Ilikuwepo haja gani ya kufikia hapo, ilhali inajulikana wazi kuwa ni ukosefu wa msukumo wa kweli, wazi na ulio wa haraka katika kushughulikia matatizo ya wazi ya wananchi!

Je, kwa CCM hii ya kuuma na kupuliza, je, kwa CCM hii ya kuongea kinyume na matendo yake, tutafika?
 
MWAKA MMOJA WA BAMBATAA BLOG.... BRAVO MALKIA
Mwandishi: Ramadhani Msangi Tarehe: 9/22/2009 09:16:00 AM | kiungo mahususi
Wiki iliyopita, blogi ya Bambataa chini ya Malkia Sophie Kessy, ilitimiza mwaka mmoja. Na katika kutimiza mwaka huo mmoja, malkia alisambaza ujumbe  ufuatao kwa wadau wake wote.

 Baaada ya Mwaka1 wa kuendesha blog inayohusu masuala mbalimbali ya wanamuziki na muziki wa kiafrica nimefanikiwa kujifunza mambo mengi sana ingawa ni kazi ngumu kwelikweli lakini namshukuru Mungu ananipa moyo wa Ku deal na watu mbalimbali.


Leo hii naomba kuitambulisha kwa Mara nyingine tena na kwa wale wasioifahamu naomba kuitambulisha blog yangu ya Bambataa,kwa wale wasioifahamu na wale ambao wanaoifahamu naomba sana tuendelee kushirikiana na kuendelea kuutanga Muziki wa Kiafrika ndani na nje ya mipaka yetu.


Kama unapenda kujua lolote kuhusu muziki au una lolote kuhusu muziki wa Africa unataka kunishirikisha ili tujalidi na wengine nao wafaidi basi nifikishie nami nitayafanyia kazi.

sophia80tz@yahoo.com lakini pia Tembelea www.africabambataa.blogspot.com kutana nami Malikia wako nikuenzi kiafrica kupitia clouds Fm the people station kuanzia saa moja mpaka saa tatu usiku kila siku jumatatu mpaka ijumaa asanteni na karibuni sana .

Pichani ni wana- NIGHT Express. Kutoka Kushoto ni : DJ BULA , DJ 2SHORT ,Malkia mwenyewe, ANTONIO NUGAZ AKA SWAHIBA PAMOJA NA MAESTRO WA MICHEZO X TR
 
THIS WAS THE DAY...
Mwandishi: Ramadhani Msangi Tarehe: 8/27/2009 11:10:00 PM | kiungo mahususi
Toka kwa mama nesi, baba mwana habari, tarehe 28 mwezi wa 8, mwaka 19...., alizaliwa mtoto ambaye baadae alikujapewa jina la Ramadhani Said Msangi.

Wakati alipokuwa mdogo, alikuwa na ndoto ya kujakuwa banker ukubwani kwake. Lakini leo hii kaishia katika uandishi na sheria. Na matarajio ya u-banker, ni kama yalifutika alipoufikia huo ukubwa. Na the way it is, hajutii chochote kile kwa kusahau u-banker na kuangukia uandishi na sheria.

Na wakati leo hii akisherehekea siku yake ya kuzaliwa, hakuna zawadi kubwa ambayo anamshukuru Mungu kwa kumpatia, zaidi ya wazazi wake, wadogo zake wote lakini zaidi ya yote, wanae Said na Shadya.

Asante baba yangu mzee Said Ramadhan na mama yangu bibi Fausta Ramadhan kwa kila mlilonitendea katika maisha yangu hadi leo hii. Mungu awape maisha marefu zaidi.

Asanteni wadogo zangu Ismail, Shabani, Seif na Hamisi, kwa sapoti, changamoto na heshima mnayonipa mimi kaka yenu. Mungu awajaze kila aina ya busara tuendelee kuwa pamoja.

Asanteni sana wanangu wazuri. Nawapenda sana maana ninyi mnachangia kwa kiasi kikubwa kuifanya dunia izunguke upande wangu.

Asanteni sana ndugu zangu wengine wote, marafiki na jamaa zangu. Nawapenda na nawaombea Mungu awajaze kila lililo jema ili muendelee kuwa msaada kwangu.

Nawapenda nyote kwa ujumla, nawaombea maisha mema na marefu ili muendelee kuniombea nami na kuwa msaada zaidi kwangu.

Najisikia nina deni kubwa katika kumshukuru Mungu kwa kunifikisha leo hii na nakuomba Allah, unijaze ujasiri na nguvu za kutenda yale uliyonikusudia wakati unaniumba na kunifikisha hapa.

Happy Birthday Rama Msangi, Happy Birthday Msangimdogo, Happy Birthday ME.
 
NANI MWINGINE WA KULIANDIKIA TAIFA HILI HISTORIA?
Mwandishi: Ramadhani Msangi Tarehe: 8/18/2009 12:11:00 AM | kiungo mahususi
Baada ya hayati Mwl. Nyerere, aliyeuhangaikia uhuru wa nchi yetu (japo ni wa bendera) na hatimae mzee Mwinyi, aliye-reintroduce mfumo wa vyama vingi japo ni chini ya robo ya Watanzania tuliokuwa tumeukubali, ni kama nchi hivi sasa imekosa watu wa kuiandikia historia upya.

Matarajio makubwa ya Watanzania yalikuwa kwa rais wa sasa, Jakaya Kikwete. Lakini wakati miaka yake mitano, ikielekea magharibi hivi sasa, hakuna hata dalili ya yeye japo kuongeza tu kurasa mpya, achilia mbali kuiandika upya.

Huyu alikuwa mtu aliyebeba imani kubwa sana ya Watanzania ambao tulitaraji kwanza kabisa angehakikisha mchakato wa kubadili/kuboresha katiba unaenda kasi ili waliotutafuna katika awamu za nyuma wanawajibishwa (maana hawawezi kujiwajibisha).

Huyu alikuwa mtu ambaye Watanzania wengi walitaraji atende katika matamshi yake, na si kutenda kinyume na kauli zake.

Huyu alikuwa mtu ambaye tulitarajia hivi sasa awe amenuniana na wanyonyaji wanaojiita wawekezaji, awe amewatimua kama si kuwawajibisha kwa kuwaibia Watanzania.

Tulitarajia kuwa awe ametekeleza ahadi yake ya kuhakikisha waisilamu hawageuki kuwa mjadala wa Bungeni hivi sasa.

Tulimtaraji awe mfano wa watakaomfuata katika kuitekeleza sheria kwa kuwawajibisha watendaji ambao wamewahujumu Watanzania kwa kutumia fedha zao kupata elimu ambayo wameiweka mifukoni mwao na kujaza tamaa vichwani mwao.

Tulimtarajia kwa mengi kwakweli, lakini inavyoonekana ni kuwa ameukosa ujasiri huo. Amekosa muda wa kupambanua tofauti baina ya Watanzania wenzake wanaomuamini dhidi ya ile ya marafiki.

Matokeo yake, hali ndio kama ilivyo. Maisha bora kwa kila Mtanzania, umekuwa wimbo ambao hauchezeki hivi sasa.

Hapa ndipo wasiwasi mkuu unapokuja na tukaanza kujiuliza. Je, hofu hii aliyonayo JK, inatokana na nini hasa? Kipi kinamshinda au wapi anakwama katika kutengua maamuzi ambayo yalifanywa awali lakini anajua wazi yanawagharimu Watanzania?

Ni kwakuwa alikuwa sehemu ya maamuzi hayo au? Na hata kama ni hivyo, je, suluhisho ni kusahihisha makosa kwa kutenda makosa zaidi?

Kama JK, anashindwa, na ndio dalili zilizopo, nani wa kuandika upya historia ya ukombozi wa Mtanzania?

Labels:

 
ukibonyeza hapa, unabakia katika blogi hii